• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC MVOMERO ATOA ONYO KALI KWA WENYEVITI WA VIJIJI, VITONGOJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Posted on: January 28th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli ameonya vikali viongozi wa vijiji na vitongoji wanaojihusisha na uchochezi wa migogoro kati ya wakulima na wafugaji, akisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na migogoro hiyo.

Mhe. Nguli ametoa onyo hilo Januari 28, mwaka huu wakati akifungua mafunzo ya utendaji kazi kwa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji pamoja na Watendaji wa Vijiji wa Tarafa za Turiani na Mvomero.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema baadhi ya viongozi wa vijiji na vitongoji wamekuwa chanzo cha migogoro hiyo kwa kushiriki kugawa ardhi kiholela, kupendelea upande mmoja, au kutoa matamko ya kichochezi huku akibainisha kuwa suala hilo hatolifumbia macho.

“…kwenye suala la migogoro ya wakulima na wafugaji sitokuwa rafiki wa mtu yeyote kwa sababu linaumiza wengi, linatia umaskini wengi…msiturudishe nyuma…” amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Nguli amesema kwa sasa Wilaya hiyo ipo kwenye harakati za kuondoa migogoro hiyo kwa kuwahamasisha wafugaji kupanda malisho na kuchimba visima kwa ajili ya mifugo yao, huku akisema kuwa uhamasishaji huo umeanza kuleta tija ambapo migogoro hiyo imepungua kwa kiasi kikubwa.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Wilaya amewataka Wenyeviti hao kwa kushirikiana na Watendaji wao wa Vijiji kuhakikisha kuwa wanasoma mapato na matumizi ya vijiji. Pia, amewataka watendaji wa vijiji na wenyeviti kufanya kazi kwa ushirikiano huku wakiepusha migogoro isiyo na tija katika utendaji kwazi wao.

Naye, Katibu Tawala Wilaya hiyo, Bw. Said Nguya amewataka wenyeviti na watendaji hao kuwa na lugha zinazoakisi dhamana waliyokuwa nayo.

Naye Bw. Stephen Mmanywa akimuwakilisha Mkuu wa Idara ya Utumishi na Rasilimali watu katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero amesema mafunzo hayo ni ya siku nne ambapo yatahitimishwa Januari 30, 2025, jumla ya wenyeviti wa vijiji 130 na wenyeviti wa vitongoji 687 watapata mafunzo hayo kwa  tarafa zote nne.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • RAS MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA "JISOMESHE NA MKARAFUU" KUWAWEZESHA WANAFUNZI KIUCHUMI

    March 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.