• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

WAHITIMU JESHI LA AKIBA WAAHIDIWA KIPAUMBELE NAFASI ZA AJIRA KATIKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA

Posted on: September 12th, 2025

Wahitimu wa Jeshi la Akiba Wilayani Mvomero wamehakikishiwa kupewa kipaumbele katika nafasi mbalimbali za ajira hususan katika vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na vyombo vingine vya usalama kwa kuzingatia sifa na vigezo vitakavyoainishwa na vyombo hivyo.


Ahadi hiyo imetolewa Septemba 12, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto wakati wa sherehe ya kufunga mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba, kundi la 10 mwaka 2025 yaliyofanyika katika Kata ya Mtibwa, Tarafa ya Turiani.


Mkuu huyo wa Wilaya amesema Serikali katika ngazi ya Wilaya itaendelea kutoa kipaumbele kwa askari wa jeshi la akiba huku akiwataka kujiendeleza katika fani mbalimbali ili kuongeza sifa za ziada za kuweza kuajiriwa.


"...niwahakikishie kuwa Serikali katika ngazi ya Wilaya itaendelea kutoa kipaumbele kwa wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la akiba katika nafasi za ajira zitakazotangazwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) au vyombo vingine vya ulinzi na usalama..." amesema Mhe. Maulid Dotto.


Aidha, Mkuu wa Wilaya ametoa wito kwa makampuni na taasisi za kiserikali kuajiri walinzi waliofuzu mafunzo ya jeshi la akiba ili kuwezesha udhibiti wa matukio na vitendo vya kiarifu ambavyo vinaweza kujitokeza katika maeneo ya makazi au biashara.


Sambamba na hilo, Mhe. Dotto ametoa rai kwa Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya kusimamia na kuhakikisha kuwa wahitimu hao wanapatiwa vyeti vyao pamoja na vitambulisho kwa wakati ili waweze kuvitumia kuomba ajira kwenye taasisi mbalimbali za Serikali na mashirika binafsi.


Kwa upande wake, Mshauri wa Jeshi la akiba Wilaya ya Mvomero Geofrey Mwakabende amesema kuwa mafunzo hayo yalianza rasmi Aprili 28,2025 yakiwa na wanafunzi 65 ambapo idadi hiyo iliongezeka hadi kufikia wanafunzi 111 huku akibainisha kuwa ongezeko hilo linatokana na uhamasishaji uliofanywa kwa kushirikiana na viongozi wa Kata na Vijiji. Aidha, ametoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi ili waweze kujiunga na mafunzo ya Jeshi hilo la akiba.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC DOTTO AZUIA ENEO LA KIJIJI LILILOUZWA KINYUME NA UTARATIBU, AAGIZA ALIYENUNUA ARUDISHIWE FEDHA ZAKE

    December 18, 2025
  • AHADI YA RAIS SAMIA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE YAANZA KUTEKELEZWA, WASIMAMIZI VITUO VYA AFYA WAJENGEWA UWEZO KUFANIKISHA

    December 18, 2025
  • DC MVOMERO ATOA SIKU SABA WAFUGAJI WALIOVAMIA SKIMU YA UWAWAKUDA KUONDOLEWA

    December 17, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA: WANANCHI WAPATA GARI LA WAGONJWA, WAISHUKURU SERIKALI KUWAONDOLEA ADHA KUSAFIRISHA WAGONJWA WA RUFAA

    December 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.