• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

NeST ITUSAIDIE KUPUNGUZA MALALAMIKO YA UCHELEWESHWAJI HUDUMA, BIDHAA - DED MVOMERO

Posted on: September 18th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Ndg. Paulo Faty amesema kuwa matumizi ya mfumo mpya wa ununuzi wa NeST (National e-Procurement System of Tanzania) ukitumika ipasavyo utasaidia kupunguza changamoto za ucheleweshaji wa huduma na upatikanaji wa bidhaa zinazohitajika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya serikali.


Ndg. Faty ameyasema hayo Septemba 18, 2025 wakati akifungua mafunzo ya mfumo wa NeST kwa watumiaji wa mfumo huo ngazi ya Halmashauri ambayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji huyo amesisitiza kuwa malalamiko ya ucheleweshaji wa huduma na bidhaa yamekuwa yakileta changamoto katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wakati huku akisema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kufahamu sheria za ununuzi pamoja na usimamizi wa mikataba hivyo, kurahisisha utoaji wa huduma na bidhaa.


Aidha, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua umuhimu wa manunuzi hivyo ameruhusu mafunzo hayo kutolewa kwa watumishi wa Halmashauri hiyo.


Kwa upande wake, Mkuu wa Kanda ya Pwani kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Bi. Vicky Mollel amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumishi na watoa huduma ili kuongeza ufanisi katika sekta ya ununuzi wa umma. Ameongeza kuwa mfumo huo unafaida mbalimbali ikiwemo uwazi katika matumizi ya fedha za umma.


Naye, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi katika Halmashauriya Wilaya ya Mvomero Bi. Aimana Nkya ameishukuru PPRA kwa kutoa mafunzo hayo huku akisema kuwa matumizi ya NeST yataongeza ufanisi na kupunguza changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa manunuzi kupitia mfumo huo.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC DOTTO AZUIA ENEO LA KIJIJI LILILOUZWA KINYUME NA UTARATIBU, AAGIZA ALIYENUNUA ARUDISHIWE FEDHA ZAKE

    December 18, 2025
  • AHADI YA RAIS SAMIA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE YAANZA KUTEKELEZWA, WASIMAMIZI VITUO VYA AFYA WAJENGEWA UWEZO KUFANIKISHA

    December 18, 2025
  • DC MVOMERO ATOA SIKU SABA WAFUGAJI WALIOVAMIA SKIMU YA UWAWAKUDA KUONDOLEWA

    December 17, 2025
  • HISTORIA YAANDIKWA: WANANCHI WAPATA GARI LA WAGONJWA, WAISHUKURU SERIKALI KUWAONDOLEA ADHA KUSAFIRISHA WAGONJWA WA RUFAA

    December 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.