Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Halima Okash akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Ndg. Phillipina Phillipo, leo wamefanya ziara ya kikazi katika Kijiji Cha Kunke kilichopo Kata ya Mtibwa Tarafa ya Turiani kwa lengo la kutatua kero za Wananchi zilizojitokeza kijijini hapo .
Miongoni mwa Kero hizo ni pamoja baadhi ya Wafugaji kuingiza mifugo katika mashamba ya ya wakulima kinyume na taratibu na kusababisha mifugo hiyo kushambulia mazao ya wakulima.
Mkuu huyo wa Wilaya ameliagiza jeshi la polisi Wilayani humo kuhakikisha wanafanya doria za mara kwa mara ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima kati ya pande hizo mbili .
Aidha Mhe. Halima Okash amewataka wanakijiji hao kufuata mpango wa matumizi bora ya ardhi uliopangwa katika maeneo hayo na kuwataka wale wote waliowauzia wafugaji maeneo kuhakikisha wanayarejesha na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima.
Pia Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza wale wote walioacha mashamba yao kuwa mashamba-pori kuhakikisha wanayasafisha hayo na kuyatumia kwa malengo yaliyokusudiwa kwani kuyaacha hivyo ndio chanzo wafugaji kuyatumia kwa ajili ya malisho.
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.