Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ) Mh Jenista Mhagama ,Jana amefanya ziara ya kikazi Wilayani Mvomero kukagua Ofisi ya Masjala ya Aridhi iliyojengwa na MKURABITA katika Kijiji cha Melela kilichopo Kata ya Melela ,Wilayani humo katika zoezi la urasilimishaji wa Aridhi ya Wananchi.
Katika ziara hiyo ambayo pia ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Halima Okash pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt. Philipina Philipo,Mh Waziri pia amegawa Hati za Kimila kwa Wananchi wa Kijiji hicho na Maeneo jirani.
Akizungumza na Wananchi Mhe. Waziri amempongeza Mkuu wa Wilaya na uongozi kwa ujumla Wilayani humo kwa usimamizi mzuri wa Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa Katika maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya hiyo ukiwamo huu wa jengo la Masjala ya Aridhi.
Pia Mhe. Waziri amewataka wananchi kutumia fursa hiyo ya urasimishaji wa maeneo yao katika Kujiinua Kiuchumi kwani Urasimishaji huo Umeongeza Kwakiasi kikubwa thamani ya Aridhi yao Kutokana na Hatimiliki hizo za Kimila walizopata na Kuwataka Kuzitunza ili ziweze kuwa na tija katika Maendeleo yao Kiuchumi.
Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo Mh Halima Okash amemshukuru Mh Waziri kwakutenga muda na kuja Wilayani Mvomero Kwaajili ya Kutembelea na Kukagua Shughuli za Maendeleo ikiwa ni Pamoja na Kugawa Hatimiliki za Kimila kwa Wananchi wa Melela.
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.