• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MFUMO WA STAKABADHI GHALANI WAPIGA HODI MVOMERO, WADAU WA KILIMO WATAKIWA KUUPOKEA

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewataka wadau wa kilimo Wilayani humo kuupokea kwa mikono miwili Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa kuwa mfumo huo utawainua wakulima na kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

Mhe. Nguli ametoa wito huo Mei 16, 2024 wakati akifungua mkutano wa Wadau wa Mfumo wa stakabadhi za ghala ili kuuza mazao ya Ufuta, Mbaazi, Alizeti na Korosho uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mvomero.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema wakulima wamekuwa hawapati faida kutokana na kuuza mazao yao kwa mifumo isiyo rasmi hali hiyo inasababisha Halmashauri kushindwa kukusanya mapato yake halisi, hivyo amewataka Waheshimiwa Madiwani, Watendaji wa Kata, Maafisa kilimo pamoja na wakulima kuukubali mfumo huo ili kuinua hali za wakulima na mapato ya Halmashauri.

“...Mvomero tuna ardhi nzuri, inarutuba, inazalisha na inatija tukitumia huu mfumo vizuri matokeo yake kwa wakulima wetu ni makubwa...” amesema Mhe. Judith Nguli.

Aidha, ameongeza kuwa mfumo huo unafaida kwa wakulima kwa kuwa utawahakikishia upatikanaji wa masoko, usalama wa mazao yao, utawaepusha na madalali ambao wamekuwa wakinunua mazao kwa bei ya chini, wakulima watakutanishwa na taasisi za kifedha na kuongeza mnyororo wa thamani kwa mazao wanayolima.

Katika hatua nyingine, Mhe. Judith Nguli amewataka wakulima Wilayani humo kujiunga kwenye vyama vya ushirika ili kuwawezesha kuuza mazao yao na kupata pembejeo za kilimo kwa urahisi.

Sambamba na hilo, amewataka Viongozi wa kisiasa Wilayani humo kutoa elimu na kuhamasisha wakulima katika maeneo yao kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani wakati wa kuuza mazao yao.

Awali wakati akisoma taarifa ya hali ya uzalishaji wa mazao ya kilimo Wilayani humo, Afisa Kilimo wa Halmshauri ya Wilaya ya Mvomero Bi. Ruth Mazengo amesema Halmashauri imepoteza mapato kiasi cha shilingi 5,000,337,878 kutokana na wakulima kuuza mazao ya Ufuta, Alizeti, Mbaazi na Korosho kwa mfumo usiyo rasmi.

Aidha, Bi. Ruth ameeleza faida zitakazopatikana ikiwa wakulima watauza mazao yao kwa mfumo wa Stakabadhi Ghalani ni Pamoja na mazao yatauzwa kwa bei halisi hivyo kuisaidia Halmashauri kupata mapato yake, upatikanaji wa masoko ya uhakika na usalama wa mazao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Yusuph Makunja amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuwa na nia ya dhati ya kuinua Halmashauri kutoka mahali ilipo sasa. Pia amemuhakikishia kuwa Waheshimiwa Madiwani wataupokea mfumo huo kwa manufaa ya Halmashauri na wakulima ambao ndiyo wa piga kura wao.

MWISHO.

 

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.