• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC NGULI AUNDA TIMU KUCHUNGUZA MGOGORO WA SHAMBA LENYE EKARI 4700 NJEULA

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ameunda timu ya wataalam kwa ajili ya kuchunguza undani wa mgogoro wa shamba lenye ekari 4700 katika Kijiji cha Njeula kilichpo Kata ya Mziha Wilayani humo ili aweze kutoa suluhisho la mgogoro huo.

Mhe. Nguli amebainisha hayo Mei 16 mwaka huu wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Njeule kwenye mkutano wa hadhara ikiwa ni ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi Wilayani humo.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema pamoja na kusoma taarifa zinazohusu mgogoro huo na kusikiliza wananchi ameunda timu ya wataalam ambao watafika kijijini hapo kwa ajili kuchunguza mgogoro huo kwa kufanya mahojiano na wananchi, mmiliki wa shamba hilo na viongozi wa Kijiji hicho, timu hiyo imepewa siku 14 kufanya uchunguzi huku akisema kuwa majibu ya ripoti hiyo itatolewa baada ya siku 21.

“...waliouza na waliouziwa wote watahojiwa na Afisa ardhi atatoa timu na mimi nitatoa timu ya maafisa watakuja hapa...ndani ya siku 14 kuanzia leo nitapewa hiyo ripoti...” amesema Mkuu wa Wilaya.

Mhe. Nguli amewataka wananchi kusitisha shughuli za kilimo katika eneo hilo lenye mgogoro isipokuwa kwa shughuli ya uvunaji pekee wakati timu hiyo ikiendelea na uchunguzi. Aidha amewataadharisha wananchi dhidi ya watu watakao tumia mgogoro huo kwa maslahi ya kisiasa na kuwataka wananchi kuwakwepa watu hao.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwaka huu.

Sambamba na hilo Mhe. Nguli ameahidi kuzifanyia kazi kero zilizoibiliwa na wananchi ili ziweze kutatuliwa.

Naye Mwenyekiti wa Kitongoji cha Lukwemzi Mhe. Zakaria Benjamini ameeleza kero ya kukosekana kwa shule ya msingi hali inayosababisha wanafunzi kutembea umbali wa kilometa 14 kwa ajili ya kupata elimu katika Kijiji cha Njeula hivyo ameiomba Serikali kusaidia umaliziaji wa vyumba viwili vya madarasa ambavyo vimejengwa kwa nguvu za wananchi ambapo ujenzi huo umefikia hatua ya lenta.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.