• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

Nyuki

KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI

LENGO KUU NA MAJUKUMU YA KITENGO

1.0.UTANGULIZI;

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kama ilivyo kwa Halmashauri nyingine nchini ilianzisha rasmi kitengo cha Ufugaji nyuki  chenye hadhi ya Idara mnamo tarehe 01/03/2014.Kitengo hiki kimeanzishwa kwa mujibu wa waraka  namba GA.215/262/01/83 wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI uliotolewa tarehe 25/06/2011 kupitia miundo  mipya ya Serikali za Mitaa iliyoidhinishwa na Mh.Waziri Mkuu tarehe 08/06/2011.Kitengo kitaendelea kutekeleza shughuli zake kwa kuzingatia Sera ya ufugaji nyuki ya mwaka 1998,Sheria namba 15 ya ufugaji nyuki ya mwaka 2002  na kanuni zake za mwaka 2004.Kimsingi hapo awali kitengo hiki kilikuwa kinawajibika chini ya Idara ya Ardhi na Maliasili mpaka kilipopatiwa hadhi husika na kuweza kujitegemea rasmi huku kikiwajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya husika.

 2.0.LENGO KUU LA KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI;

Kuongeza mchango wa sekta ya ufugaji nyuki kwa maendeleo endelevu ya ukuaji wa uchumi wa jamii ya Wilaya ya Mvomero na kuboresha uhifadhi na usimamizi wa maliasili zake kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

3.0.MAJUKUMU YA KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI

3.1.Kuongeza uwezo wa Wilaya kusimamia na kuendeleza sekta ya ufugaji nyuki kwa kushirikiana na wadau mbali mbali k.m Wakulima,Jumuiya za wananchi(CBOs),Wafugaji nyuki,Sekta binafsi,Serikali kuu,Asasi zisizokuwa za kiserikali na Jumiya za kimataifa pia.

3.2.Kuboresha uhifadhi wa bioanuai,kuongeza ajira na pato la kaya kwa jamii na hatimaye Taifa kutokana na maendeleo ya biashara ya mazao ya nyuki k.m asali,nta n.k

3.3.Kuwezesha kuongezeka kwa ubora na upatikanaji endelevu wa mazao ya nyuki  kupitia kilimo mseto ambapo uchavushaji wa maua unaleta ufanisi wa chavua na mbochi.

3.4.Kuhakikisha kuwapo kwa nyuki wa asali kwa kufanya yafuatayo;

i)Kuihimiza jamii kupitia viongozi mbali mbali kujiepusha na uchomaji moto ovyo misitu ili kutunza misitu ambayo ni chimbuko kubwa la maua ya kuzalisha mazao ya nyuki

ii)Kuanzisha hifadhi za nyuki(Bee reserves) zitakazosimamiwa kikamilifu na jamii husika

3.5..Kushiriki katika shughuli za uhifadhi misitu hususani Usimamizi shirikishi wa misitu(kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya misitu(1998),Sheria namba 14 ya mwaka 2002 na Kanuni zake za mwaka 2004)  ili kuwezesha upatikanaji endelevu wa maua kwa ajili ya mbochi(Nectar) na chavua(pollen)

 3.6.Kuratibu huduma za ugani wa ufugaji nyuki kadri zinavyohusiana kwa karibu na sekta nyingine k.m wanyamapori,misitu,killimo n.k.

3.7.Kuanzisha,kusimamia na kuendesha hifadhi za nyuki zitakazokuwa zimeanzishwa kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya ufugaji nyuki ya mwaka 1998,Sheria namba 15 ya mwaka 2002 na Kanuni zake za mwaka 2005 na pia fursa zilizopo k.m.ufadhili n.k

3.8.Kushirikiana na Idara ya maendeleo ya jamii katika shughuli za uhamasishaji ikiwa ni pamoja na kuhakikisha usajili wa kisheria wa vikundi na mashirika ya kijamii(CBOs) vinavyojihusisha na ufugaji nyuki unafanikiwa.

3.9.Kushirikiana na sekta ya Ushirika katika kuhakikisha kuwa vikundi vyenye sifa stahiki vinaanzisha ushirika wa kuweka na kukopa(Saccos) wa wafugaji nyuki ili kumudu gharama za uzalishaji mazo ya nyuki na hivyo kuipunguzia Serikali jukumu za kuviwezesha kupitia raslimali fedha,vifaa n.k.

Imetolewa na;

T.D.MWAIKENDA

Mkuu wa Kitengo cha Ufugaji nyuki

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

Matangazo

  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA KWA MWAKA WA MASOMO 2021 December 18, 2020
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA (JOINING INSTRUCTION) KIDATO CHA KWANZA 2021 KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA HALMASHAURI December 15, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI LEO 6/09/2017 September 06, 2017
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI December 12, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • JUMLA YA KAYA 6172 ZA WANUFAIKA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI (TASAF III) WILAYANI MVOMERO WAMEPOKEA KIASI CHA SHILINGI MIL. 288,888,000/= AWAMU YA 25

    March 02, 2021
  • Mkurugenzi Mtendaji Awaagiza Maafisa Mifugo Kubadilika na Kukaa Kwenye Vituo Vyao Vya Kazi.

    February 17, 2021
  • Mh.Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Aagiza wawekezaji kujitokeza kwa wingi Kujenga Viwanda Vya kuzalisha Sukari

    February 16, 2021
  • Mkuu Wa Wilaya Apokea na Kugawa Vifaa Vya Msaada Kwa Waathirika wa Mvua na Upepo mkali Vijiji Vya Kipera na Kinyenze

    January 14, 2021
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.